• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

Posted on: August 21st, 2024

Na: Nassoro Rashid - Mkingadc Habari

Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mhe. Gilbert Kalima ametoa wito kwa Mashirika yasiyo ya Kiserikali kushirikiana na Serikali katika kupiga vita vitendo vya ukatili wa kijinsia, matumizi ya madawa ya kulevya, ubakaji pamoja na ulawiti kwa jamii.

Mhe. Kalima ametoa wito huo Agosti 21, 2024 wakati alipokuwa akifungua Jukwaa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri.

Akizungumza kwa msisitizo Mkuu wa wilaya amesema kazi ya kupiga vita matendo yanayokiuka maadili ni jukumu la wote hivyo ameroa wito kwa Mashirika hayo kushirikiana na serikali ili kuijenga Mkinga isiyo na tabia za ukiukwaji wa maadili.

"Kumekuwa na matukio mbalimbali ya ukatili wa kijinsia, matumizi ya madawa ya kulevya, ubakaji na ulawiti yanayokiuka sheria za nchi, naomba tuongeze nguvu katika kusimamia suala zima la maadili ili kuijenga jamii yetu katika misingi iliyo bora na inayomcha Mungu, tupige vita kwa nguvu zetu zote ili kuondokana na tabia hizi". Alisema Mhe. Kalima.

Aidha Mhe. Kalima amesema hawawezi kupuuza juhudi na kazi kubwa zinazofanywa na mashirika hayo katika kuwafikia Wananchi kupitia sekta mbalimbali na kuahidi kuwa serikali ipo tayari na itaendelea kushirikiana nao ili kuhakikisha dhana ya maendeleo endelevu inatafsiriwa ipasavyo kwa wananchi.

"Nipende kuchukua nafasi hii kuwapongeza sana kwani nyinyi mmekuwa wadau wakubwa wa maendeleo katika wilaya yetu, tupo tayari kuendeleza ushirikiano huu ili kuhakikisha malengo ya kazi zilizopangwa kwa wilaya ya Mkinga zinafanikiwa". Alisema Mhe. Kalima.

DC Kalima amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri kwa wadau wa maendeleo yakiwemo mashirika hayo kwenye utekelezaji wa shughuli zao ikiwa ndio ishara nzuri na upendo wa Mhe. Rais kwa Wananchi wake wa Tanzania.

Jukwaa hilo hufanyika kila mwaka kisheria ambapo viongozi wa Mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na wataalam hukaa pamoja na kujadili uwasilishwaji wa taarifa za utendaji kazi na kubadilishana uzoefu, pia kupata fursa ya kujadili mafanikio makubwa ambayo yamepatikana kupitia juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa maendeleo.

#Kaziiendelee


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • BARAZA LA MADIWANI, MKURUGENZI MTENDAJI, WATAALAM NA WATUMISHI WOTE WANAKUKARIBISHA MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLAH HALMASHAURI YA (W) MKINGA

    August 16, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017