• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

Posted on: August 20th, 2024

Na: Nassoro Rashid - Mkingadc Habari

Wito umetolewa kwa jamii ya wilaya ya Mkinga kuchukua tahadhari dhidi ya homa ya nyani ambao ni ugonjwa wa mlipuko unaosababishwa na kirusi aina ya Mpox.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mhe. Gilbert Kalima Agosti 20, 2024 wakati akiongoza kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa wilaya.

Kikao hicho kilichojumuisha Kamati ya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Dini, Kamati ya wataalam ya Halmashauri, Wataalam wa Afya, Wazee Maarufu pamoja na Maafisa Tarafa.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Kalima amesema kila mtu kwa nafasi yake anapaswa kuchukua tahadhari kwa kutoa elimu kwa jamii ili kuhakikisha Wananchi wanajengewa uelewa wa kutosha ili kuepukana na ugonjwa huo.

"Niwaombe kila mmoja wetu kwa nafasi yake kuanzia Viongozi wa Dini, Vijiji, Kata, Kamati za ulinzi na Usalama, Madiwani, Walimu, Wataalam wa afya pamoja na Wananchi kwa umoja wetu kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huu, tunapaswa kutoa elimu hii kwa Jamii ili kujengeana uelewa zaidi kwani Mkinga ni moja ya Wilaya zilizopo mpakani hivyo tukishirikiana vizuri tutafanikiwa kuudhibiti". Alisisitiza Mhe. Kalima.

Aidha Mhe. Kalima amesema kwa pamoja wameazimia kuwa elimu iendelee kutolewa kuhusu dalili na namna ya kujikinga na ugonjwa kupitia wataalam wa afya, pili viongozi wa dini kutoa elimu kwa wananchi maeneo ya ibada, elimu kutolewa mashuleni ili wanafunzi wafikishe ujumbe huo kwa Wazazi na Walezi pamoja na matangazo kwa umma.

Kadhalika Halmashauri kuweka mikakati ya ujenzi wa zahanati ya Horohoro pamoja na kutenga bajeti ya dharula kwa ajili ya utayari wa udhibiti mzuri wa ugonjwa huu.

Naye Kaimu Mganga Mkuu Dkt. Castory Chuwa amesema virusi vya Mpox kawaida hushambulia panya au nyani na unaweza pia kumshambulia binadamu.

Pia ameongezea kuwa ugonjwa huu umetolewa taarifa katika nchi za Afrika ya kati na Magharibi na visa vingi katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara Afrika  kutokana na uwepo wa  mwingiliano wa wasafiri (Binadamu, Wanyama na bidhaa mbalimbali) kutoka mataifa mbalimbali.

#Kaziiendelee



Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • BARAZA LA MADIWANI, MKURUGENZI MTENDAJI, WATAALAM NA WATUMISHI WOTE WANAKUKARIBISHA MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLAH HALMASHAURI YA (W) MKINGA

    August 16, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017