• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

DC KALIMA KUJA NA MKAKATI SHIRIKISHI WA KUINUA ZAO LA KOROSHO MKINGA

Posted on: September 30th, 2025

Na: Nassoro Rashid – Mkinga

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mhe. Gilbert Sylvester Kalima, amesema serikali wilayani humo imejipanga kuanzisha mkakati shirikishi wa kuinua zao la korosho kwa kushirikiana na wananchi, viongozi wa vijiji na wataalamu wa kilimo, ili kuongeza uzalishaji na tija kwa wakulima.


Mhe. Kalima aliyasema hayo Septemba 30, 2025 wakati akiongoza ziara ya kamati ya ulinzi na usalama akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, Ndugu Rashid Gembe, pamoja na kamati ya wataalamu kukagua miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika wilaya hiyo.


Alisema korosho ni zao la kimkakati linaloweza kuchochea uchumi wa Mkinga, hivyo ipo haja ya kuweka mpango maalum wa kuwasaidia wakulima kuondokana na changamoto zinazowakabili, ikiwemo upatikanaji wa pembejeo bora, elimu ya kitaalamu ya kilimo bora na uhakika wa masoko.


“Tunataka mkakati huu uwe shirikishi, maana yake wananchi wenyewe washirikishwe tangu hatua za awali za kupanga hadi kutekeleza. Tukiwa na ushirikiano wa karibu kati ya serikali, wataalamu na wakulima, tutaweza kulifanya zao la korosho kuwa uti wa mgongo wa uchumi wa Mkinga,” alisema DC Kalima.

Aidha Mhe. Kalima alisisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa wakulima na wananchi kuhusu zao la korosho, akieleza kuwa baadhi yao wamekuwa wakiliacha zao hilo kutokana na mitazamo potofu na changamoto za muda mrefu zilizowahi kujitokeza.


“Tunataka mkakati huu usibaki kwenye karatasi pekee, bali uende sambamba na elimu ya mara kwa mara kwa wakulima wetu. Wengi wamekuwa wakiliacha zao hili wakidhani halina tija, kumbe tatizo ni ukosefu wa mbinu bora na maarifa ya kilimo cha kisasa. Tukiwapa elimu sahihi, mitazamo yao itabadilika na wataona thamani kubwa ya zao hili,” alisema DC Kalima.


Alibainisha kuwa elimu hiyo itatolewa kupitia maafisa ugani, mikutano ya vijiji, pamoja na vikundi vya wakulima ili kuhakikisha kila mkulima anafikiwa na kupata uelewa wa kutosha.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Rashid Gembe, alisema mpango huo utahusisha pia uhamasishaji wa matumizi ya miche bora ya kisasa badala ya mashamba pori yaliopo sasa na kuimarisha usimamizi wa vyama vya ushirika ili kuhakikisha wakulima wananufaika moja kwa moja na mazao yao.


Mkakati huo unatarajiwa kuongeza uzalishaji wa korosho wilayani Mkinga na kuchochea mapato ya serikali na kaya, sambamba na kufungua fursa mpya za biashara kwa wananchi.


Ziara hiyo ilihusisha ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa ghala la korosho lenye uwezo wa kuhifadhi zaidi ya tani 10,000, kutembelea kikundi cha kinamama wachakataji wa mhogo Mtimbwani, wanufaika wa TASAF kijiji cha Tawalani, pamoja na maendeleo ya ujenzi wa soko la samaki Moa.

#mkingakaziinaendelea

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC KALIMA KUJA NA MKAKATI SHIRIKISHI WA KUINUA ZAO LA KOROSHO MKINGA

    September 30, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017