• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

"MIMIAKA 62 YA UHURU WILAYA YA MKINGA IMEPIGA HATUA YA MAENDELEO" - MHE. KANALI SURUMBU

Posted on: December 9th, 2023

Na: Nassoro Rashid - MDC Habari

Kauli hiyo imesemwa Disemba 9, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Mhe. Kanali Maulid Hassan Surumbu wakati akihutubia Wananchi katika maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru kiwilaya yaliyofanyika katika Ukumbi uliopo makao makuu ya ofisi za Halmashauri.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mhe. Surumbu amesema kuna kila sababu ya kuendelea kuuenzi uhuru wa nchi yetu kulingana na maendeleo mbalimbali yaliyofikiwa kupitia awamu mbalimbali za viongozi tangu mwaka 1961 hadi sasa huku akielezea kuwa wilaya ya Mkinga ilikuwa na mchango katika kupigania uhuru huo.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ametanabaisha kwamba serikali ya wilaya ya Mkinga kwa kushirikiana na Wananchi imepiga hatua ya maendeleo katika miaka 62 kutokana na utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo kabla ya uhuru haikuwepo.

"Miaka 62 ya Uhuru Wilaya ya Mkinga imepiga hatua ya maendeleo katika nyanja tofauti ikiwemo sekta ya afya, kabla ya uhuru hatukuwa na vituo vya afya lakini sasa tunavyo 43, tulikuwa na shule za msingi 15 na sasa tunazo 85, hatukuwa na shule za sekondari lakini sasa tunazo 17,  kadhalika sekta ya kilimo kumekuwa na ongezeko la mazao ya korosho, mkonge na viungo, pia tumepiga hatua sekta ya nishati ambapo Mkinga kwa sasa inapokea umeme kutoka gridi ya Taifa". Alisema Mhe. Kanali Surumbu.

Sambamba na hayo Mhe. Surumbu ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuilinda amani na mshikamano uliopo huku akiwataka vijana kufanya kazi kwa bidii kwa kutumia fursa zilizopo kuiletea zaidi maendeleo wilaya ya Mkinga.

Maadhimisho hayo yaliohudhuriwa na makundi mbalimbali ya watu ikiwemo kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Wazee maarufu waliokuwepo kipindi cha Uhuru, Watumishi, Wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari pamoja na Wananchi yamekuwa ni sehemu ya kuhitimisha sherehe hizo mara baada ya shughuli mbalimbali kufanyika tangu Disemba 1, 2023 ikiwemo kufanya usafi wa Mazingira, Bonanza la Michezo, Mashindano ya uandishi wa Insha kwa Wanafunzi pamoja na upandaji wa miti.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • BARAZA LA MADIWANI, MKURUGENZI MTENDAJI, WATAALAM NA WATUMISHI WOTE WANAKUKARIBISHA MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLAH HALMASHAURI YA (W) MKINGA

    August 16, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017