• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

MFUKO WA ABBOTT KUFADHILI BILIONI 8.9 KUKARABATI NA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SHULE YA SEKONDARI MAPATANO WILAYA YA MKINGA

Posted on: July 12th, 2023

Na. Nassoro Rashid

       MDC Habari

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof.Adolf Mkenda (Mb) kwa kuambatana na mgeni wake Rais wa Mfuko wa ABBOTT Duniani Bi. Melissa Brotz Julai 12, 2023 wamezindua mradi mkubwa wa ukarabati na uboresha wa miundombinu ya Shule ya Sekondari Mapatano iliyopo wilaya ya Mkinga.

Mara baada ya uzinduzi Mhe.Waziri Mkenda amesema mradi huo unaofadhiliwa na Mfuko wa Abbott utagharimu zaidi ya

shilingi Bilioni 8.9 hadi kukamilika kwake na kuifanya shule ya Mapatano kuwa ya mfano Mkoani Tanga.

"Mradi huu unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 12 ambapo utahusisha majengo zaidi ya thelathini (30), ni imani yangu kwamba shule hii inakwenda kuwa ya mfano mkoa wa Tanga kutokana na maboresho yake pamoja na kujengwa kwa miundombinu ya madarasa yote yaliyopo sambamba na kujenga madarasa mapya ya kidato cha tano na sita, maabara za kisasa, mabweni, viwanja vya michezo pamoja na ujenzi wa nyumba za walimu". Alisema Mhe. Waziri Mkenda.

Naye Rais wa Mfuko wa Abbott Duniani Bi.Melissa amesema wanafahamu kwamba kuboresha miundombinu ya elimu ni sehemu ya kuimarisha

maendeleo yake hivyo hawatoacha kuendelea kufadhili miradi ya elimu ili maono ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yatimie ya kuhakikisha Wananchi wote wanapata elimu bora pamoja na kuboresha maisha  yao kwa kuleta maendeleo nchini.

Sambamba na hayo Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Mhe. Kanali Maulid Hassan Surumbu ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe.Waziri Kindamba alisema,

"Uwepo wa wadau mbalimbali wa maendeleo katika Mkoa wa Tanga na leo Wilaya ya Mkinga ni matunda ya kazi nzuri inayofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuifungua Tanzania, hivyo hatuna budi kuendelea kumuunga mkono na kumshukuru kwa jitihada hizi

ambazo zinaendelea kuinufaisha wilaya hii kupitia uboreshwaji wa miundombinu ya elimu lakini pia na sekta nyingine kwa ustawi mpana wa maendeleo ya Wananchi". Aliongezea Mhe. Kanali Surumbu.

Shughuli hiyo pia ilihudhuriwa na Wajumbe wa Kamati ya Usalama Wilaya, Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Mbunge wa Jimbo la Mkinga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kwa sasa Mhe.Dunstan Kitandula, Mwenyekiti wa Halmashauri, Diwani wa Kata ya Mapatano na Viongozi mbalimbali wa Wilaya,Kata na Kijiji.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • BARAZA LA MADIWANI, MKURUGENZI MTENDAJI, WATAALAM NA WATUMISHI WOTE WANAKUKARIBISHA MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLAH HALMASHAURI YA (W) MKINGA

    August 16, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017