• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA TANGA MHE. SEKIBOKO ARIDHISHWA NA UJENZI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYA YA MKINGA

Posted on: July 8th, 2024

Na: Nassoro Rashid - Mkingadc Habari

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mhe. Husna Juma Sekiboko aridhishwa na ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa wilayani Mkinga.

Ameyasema hayo wakati akihitimisha ziara yake ya kutembelea wilaya 9 za mkoa wa Tanga Julai 08, 2024 ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake aliojiwekea kusikiliza changamoto za Wananchi anaowawakilisha, kutembelea miradi pamoja na kuimarisha ujenzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

"Hii ni wilaya yangu ya tisa katika ziara yangu hii ambapo leo nahitimisha kwa kufanikisha kupita kila Tarafa, hapa Mkinga nilianza Maramba na leo ni tarafa ya Mkinga, katika maeneo yote niliyopita nimeshuhudia miradi mbalimbali ikiwemo ya afya, elimu, maji, biashara, barabara, ambayo inagusa maendeleo ya Mwananchi wa Tanzania, hakika haya ndio maendeleo tunayoyataka". Alisema Mhe. Sekiboko

Aidha Mhe. Sekiboko ameipongeza Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kushusha fedha nyingi katika Halmashauri zote za mkoa wa Tanga na kufanikisha kutekeleza miradi hiyo.

"Nimeshuhudia vituo vya afya vingi, zahanati na hapa Mkinga nimeshuhudia hospitali ya wilaya yenye majengo mazuri

na yanavutia, bado mengine yanaendelea kujengwa, inaonesha kwa kiasi kikubwa thamani ya fedha imeendana na thamani ya mradi, niwapongeze viongozi wote na wataalamu kwa kusimamia utekelezaji huu". Aliongezea Mhe. Sekiboko

Kadhalika Mbunge huyo amewaomba viongozi pamoja na wataalamu kuendelea kumsaidia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwahudumia wananchi kwa kutatua changamoto zao na kusimamia utekelezaji wa sera kwa vitendo ili kuendelea kuongeza kasi ya maendeleo ya nchi yetu.

Pamoja na hayo ziara hiyo imekuwa na tija kwa Mhe. Sekiboko hususani katika kuendelea kuhamasisha Wananchi kupitia mikutano ya hadhara kwa kuwa tayari kushiriki katika uandikishaji wa daftari la

mpiga kura lililoboreshwa utakapoanza na uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.

 

#Kaziiendelee

 

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • BARAZA LA MADIWANI, MKURUGENZI MTENDAJI, WATAALAM NA WATUMISHI WOTE WANAKUKARIBISHA MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLAH HALMASHAURI YA (W) MKINGA

    August 16, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017