• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

MAAFISA MAENDELEO YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA WAKUTANA KUIMARISHA UTENDAJI KAZI NA UKUSANYAJI WA MAREJESHO YA MIKOPO YA 10%.

Posted on: November 1st, 2023

Na: Nassoro Rashid

       MDC Habari

Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Mkinga Bi. Elizabeth Malali Novemba 01, 2023 amekutana na Maafisa Maendeleo Jamii kutoka katika Kata 18 ikiwa ni kuendeleza mikakati ya uimarishaji wa utendaji kazi pamoja na kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa marejesho ya mikopo ya 10% iliyotokana na mapato ya ndani.

Akizungumza wakati wa kikao hicho Bi. Elizabeth amesema kupitia idara hiyo wameweza kufanikiwa kutekeleza shughuli mbalimbali ikiwemo uhamasishaji wa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu kupitia Dawati la uwezeshaji Wananchi kiuchumi hususani katika Mikopo ya 10%.

"Tangu kuanza kwa mikopo hii Halmashauri imefanikiwa kutoa shilingi 652,004,381 kupitia mapato yake ya ndani kwa makundi 145, hadi sasa tumefanikiwa kurejesha shilingi 258,391,943 na bakio la deni ni shilingi 375,612,438, ambapo kati ya deni hilo shilingi 68,290,638 ni fedha ya vikundi vilivyopo nje ya mkataba na shilingi 286,321,800 ni fedha zilizopo ndani ya mkataba, dhamira kubwa ya serikali ni kuhakikisha mikopo hii inarejeshwa, hivyo sisi kama Idara tumeendelea kufanya jitihada za ufuatiliaji katika kipindi cha Robo hii na tumeweza kukusanya shilingi milioni 18, 000,000 kwa vikundi vilivyo nje ya mkataba". Alisema Bi. Elizabeth

Aidha Bi. Elizabeth amesema kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wameweza kuwapata wanufaika 6231 kupitia kuunda vikundi vya kuweka akiba na kuwekeza 294 kwa vijiji 84 ambapo Wanachama katika vikundi hivyo ni 3766 ikiwemo Wanawake 3410 na Wanaume ni 356.

"Lengo la utekelezaji huu ni kuhakikisha kwamba uwezeshaji Wananchi kupitia miradi ya TASAF unaleta matokeo chanya kwenye familia katika kuongeza kipato, na lengo la kuunda vikundi kwa wanufaika huwasaidia kubuni miradi mbalimbali pamoja na kuweka akiba za fedha zao ili kuona manufaa ya fedha hizo katika kuwainua kiuchumi." Alisema Bi. Elizabeth

Pia ameongezea kuwa kikao hicho kililenga kuangalia miongozo mbalimbali inayotolewa na serikali ikiwemo uundaji wa Mabaraza ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Mabaraza ya Watoto na miongozo mingine ya Idara ili kuhakikisha Maafisa hao ngazi ya Kata Wanaunda mabaraza hayo ili Wananchi waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Naye mratibu wa TASAF wilaya Ndugu. Benson Ogada amewasisitiza maafisa maendeleo kata kuhakikisha Mashirika yote yaliyopo kwenye Kata zao yatambulike kuanzia ngazi hiyo mpaka Wilaya lakini pia mpango kazi wa mashirika hayo ufikishwe kwa maafisa hao ili waweze kujua kazi wanazojihusisha nazo kwa maslahi mapana ya ustawi mzuri wa jamii ya Wanamkinga.

Kikao hicho ni muendelezo wa vikao vya idara kila ifikapo robo mwaka vikiendelea kuwa na dhamira chanya ya kuhakikisha jamii inaendelea kuhamasishwa katika shughuli za kimaendeleo kupitia tathmini ya pamoja ya utendaji kazi ili kuendeleza mikakati ya kuimarisha shughuli mbalimbali za idara katika kuhakikisha dhana ya maendeleo ya jamii inafikiwa kwa vitendo.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • BARAZA LA MADIWANI, MKURUGENZI MTENDAJI, WATAALAM NA WATUMISHI WOTE WANAKUKARIBISHA MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLAH HALMASHAURI YA (W) MKINGA

    August 16, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017