• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

ASIBAKI MTOTO NYUMBANI KWA KISINGIZIO CHA MWANAFUNZI AMEKOSA SARE - DC SURUMBU

Posted on: January 8th, 2024

Na: Nassoro Rashid - MDC Habari

Kauli hiyo imesemwa Januari 08, 2024 na Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mhe. Kanali Maulid Hassan Surumbu mara baada ya kutembelea shule za msingi, awali na sekondari kuona mapokeo ya wanafunzi katika muhula mpya wa masomo ulioanza siku ya Jumatatu ya wiki hii.

Katika ziara yake hiyo Mhe. Surumbu amesema mwamko wa wanafunzi  kuhudhuria kwenye shule hizo umekuwa ni mkubwa sana kwa siku ya kwanza hivyo ameendelea kutoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha kila mtoto mwenye sifa anapelekwa shule.

"Mkinga ina Shule za Msingi 87 na Sekondari  17, shule zote zimefunguliwa wiki hii, tunashukuru mwitikio wa wanafunzi kwa mwaka huu umekuwa ni wa kuridhisha kutokana na uhamasishaji shirikishi kutoka ngazi ya Kitongoji hadi Wilaya, malengo ya Wilaya ni kuhakikisha kila mtoto aliyefikia umri wa kuanza Shule anaandikishwa na si vinginevyo, hivuo Mtoto mwenye umri wa miaka 5 aandikishwe shule ya Awali na wa miaka 6 Darasa la Kwanza" alisema Mhe. Kanali Surumbu

Aidha Mkuu huyo wa wilaya ametoa wito kwa viongozi kuanzia ngazi ya Tarafa hadi Vijiji kupita kila nyumba ili kuona kama kuna mtoto hajapelekwa shule hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa mzazi au mlezi wa mtoto huyo.

"Wito mwingine natoa kwa viongozi wa Tarafa, Kata, Vitongoji na Vijiji kuhakikisha wanapita nyumba kwa nyumba ifikapo Tarehe 10,2024, kila mzazi mwenye mtoto ambaye anastahili kwenda shule aende shule na kama hafanyi hivyo hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa mzazi husika, na asibaki mtoto nyumbani kwa kisingizio cha mwanafunzi amekosa sare, apelekwe shule ili aanze masomo pamoja na wenzake". Alisisitiza Mhe. Surumbu.

Pia Mhe. Kanali Surumbu amesema shule ambazo zimeendelea kujengwa kwenye wilaya ya Mkinga kupitia miradi mbali mbali takribani 19 ikiwemo pochi ya mama, Boost na miradi mingine inayowezeshwa na Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imejengwa kwa kuzingatia huduma ya watoto wenye mahitaji maalumu hivyo pia amewataka wazazi kuwapeleka shule watoto hao ili waweze kupata elimu.

"Watoto wote wenye mahitaji maalum nao wanatakiwa kuripoti kwenye shule hizi, walimu kwa ajili ya kuwafundisha wameshaandaliwa na wapo tayari, kila mzazi au mlezi anayeishi na mtoto mwenye mahitaji maalum asikae naye nyumbani na asimfiche, ahakikishe anamtoa ili aweze kupata haki yake ya elimu". Aliongezea Mhe. Surumbu..

Elimu imekuwa ni msingi muhimu wa maisha kwa binaadamu kwani imeweza kusaidia sana kwa kiasi kikubwa kuijenga Tanzania ya leo na Dunia ya sasa tunayoiona hivyo wananchi hususani wazazi na walezi wanaendelea kuhimizwa kuhakikisha wanawapa kipaumbele watoto wao kupata elimu ili ije kuinufaisha jamii kimaendeleo kadhalika kuimarisha ustawi bora wa Nchi yetu.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WITO WATOLEWA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPIGA VITA UKATILI WA KIJINSIA, MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA ULAWITI (W) MKINGA

    August 21, 2024
  • JAMII YAASWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI WILAYA YA MKINGA

    August 20, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA MAALUM LA KUPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA SHERIA NDOGO ZA UHIFADHI WA BAHARI (BMU)2024

    August 20, 2024
  • BARAZA LA MADIWANI, MKURUGENZI MTENDAJI, WATAALAM NA WATUMISHI WOTE WANAKUKARIBISHA MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLAH HALMASHAURI YA (W) MKINGA

    August 16, 2024
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017