• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

KIKAO CHA TATHMINI YA ELIMU NA MAGEUZI YA UBORA WA TAALUMA KWA WANAFUNZI MKINGA

Posted on: March 2nd, 2026

Na: Grace Melleor – Mkinga

Kikao cha tathmini ya elimu kilichowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo kimefanyika leo Machi 2, 2026 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, Mkoa wa Tanga, kikilenga kuibua mikakati mipya ya kuleta mageuzi ya ubora wa taaluma na kuinua viwango vya ufaulu kwa wanafunzi wilayani humo.

Akifungua kikao hicho, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Gilbert Kalima, amesema tathmini hiyo ni hatua muhimu katika safari ya maboresho ya elimu, kwani inatoa nafasi ya kuchambua mafanikio, kubaini changamoto na kuweka mikakati ya pamoja ya kuimarisha taaluma.

Amesisitiza kuwa mageuzi ya elimu hayawezi kupatikana bila ushirikiano wa wadau wote wakiwemo walimu, wazazi, viongozi na jamii kwa ujumla, akibainisha kuwa elimu bora ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

“Kupitia kikao hiki tunataka kuona mabadiliko ya kweli katika ubora wa taaluma. Tujadili kwa uwazi changamoto zilizopo na tupate suluhu za kudumu kwa manufaa ya wanafunzi wetu,” amesisitiza Mhe. Kalima.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Awali na Msingi (W), Ndugu Omari Mashaka, amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026 jumla ya Shilingi 982,507,846 zimetumika kutekeleza miradi ya maendeleo ya elimu, ikiwemo ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya shule. Amesema uwekezaji huo umeweka mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia, hatua inayochochea mageuzi ya taaluma.

Naye Afisa Elimu Sekondari (W), Bi. Mary Sanga, ameeleza kuwa Halmashauri imeongeza idadi ya shule za sekondari kutoka 15 mwaka 2023 hadi kufikia 21 mwaka 2026. Aidha, walimu wapya 37 wa masomo ya Sayansi, Lugha, Sanaa na Biashara wamepokelewa, jambo linalotarajiwa kuongeza ufanisi wa ufundishaji na kuimarisha matokeo ya wanafunzi.

Mdhibiti Ubora wa Elimu (W) Bi. Rosemary Thoran amebainisha kuwa tathmini ya matokeo ya mitihani ya Taifa kwa mwaka 2025 inaonesha mwelekeo chanya, ambapo ufaulu wa Darasa la IV umeongezeka kwa asilimia 1.5 na Kidato cha Nne kuongezeka kwa asilimia 2 kutoka asilimia 91.4 mwaka 2024 hadi asilimia 93 mwaka 2025.

Ameeleza kuwa ongezeko hilo ni matokeo ya juhudi za pamoja za walimu, wanafunzi na wadau wa elimu.

Kikao hicho kilichobeba kaulimbiu isemayo “Elimu Bora kwa Mtoto ni Jukumu Letu Sote” kinatajwa kuwa chachu ya mageuzi ya ubora wa taaluma katika Wilaya ya Mkinga, huku mipango ikiwekwa ya kuendeleza tathmini za mara kwa mara ili kuhakikisha maboresho yanakuwa endelevu na yenye matokeo chanya kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla.


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA KWA AMANI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 23, 2025
  • MAKARANI WAOMNGOZAJI WAPIGA KURA WAASWA KUWA WAADILIFU

    October 25, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017