Mkinga, Januari 30, 2026 – Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, Dkt. Salvio Wekesi, amewahimiza watumishi kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa mapato ili kuiwezesha Halmashauri kutekeleza kikamilifu mipango na malengo yake ya maendeleo.
Akihutubia Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa kupitisha Bajeti ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2026 - 2027 uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri, Dkt. Wekesi amesema kiwango cha ukusanyaji wa mapato ndicho kitakachoamua utekelezaji wa vipaumbele vilivyopangwa, akisisitiza kuwa ukusanyaji mzuri utaongeza ustawi na motisha kwa watumishi wote.
Ameeleza kuwa bajeti ya mwaka ujao ina fursa kubwa kwa Halmashauri endapo mapato yatakusanywa ipasavyo, jambo litakalowanufaisha watumishi na wananchi kwa ujumla. Baada ya hotuba yake, Dkt. Wekesi aliahirisha mkutano huo hadi wakati mwingine.

Kasera, Tanga -HorohoroRoad
Postal Address: P O Box 6005 Tanga
Simu: +255 027-2660501
Simu: +255 684 625 299
Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz
Mkinga dc @ 2017